Zitto Kabwe aongoza kwa wafuasi wengi mtandaoni




Dar es Salaam. Matumizi ya mitandao ya kijamii yanaongezeka kila kukicha na kuleta upinzani kwa vyombo vya habari. Hii inatokana na ukweli kwamba kupitia mitandao hiyo habari husambaa kwa haraka katika muda mfupi.
Watu wengi duniani wanatumia mitandao tofauti ya kijamii huku wanamuziki na wanamichezo wakiongoza katika orodha ya kila mtandao duniani bila kuwaacha wanasiasa.
Ndiyo maana;‘dunia ilisimama’, baada ya mtandano wa facebook kutoingilika Jumanne ya Januari 27, mwaka huu. Mamilioni ya watumiaji wa mtandao huo walikumbwa na wasiwasi wa kuvamiwa kwa mtandao huo. Kwa muda wa dakika 40, hakuna aliyeweza kuingia katika akaunti yake asubuhi ya siku hiyo.
Hitilafu hiyo ilisababisha wateja wa mtandao wa Instagram pia kukosa huduma. Hiyo ni kwakuwa mtandao huo upo chini ya kampuni ya facebook. Uongozi wa kampuni hiyo ulilazimika kutoa maelezo ya kilichotokea.
Msemaji wa facebook alikaririwa na Shirika la Utangazaji Uingereza (BBC) akifafanua juu ya hitilafu za kiufundi zilizojitokeza ili kuondoa wasiwasi uliokuwepo miongoni mwa wateja wake kwamba mtandao huo umevamiwa.
Msemaji huyo alibainisha kuwa tatizo lililojitokeza lilisababishwa na mabadiliko yaliyofanywa na mafundi kabla ya kuathiri mfumo mzima. Lakini lilitatuliwa baada ya muda mfupi. Huduma ya mitandao hiyo haikupatikana kwa muda wa dakika 40, duniani kote.
Hiyo inaonyesha ni kwa namna gani mitandao hii imekuwa muhimu katika jamii ya sasa. Mchango wake umekuwa muhimu sana katika maisha ya wanamuziki na wanamichezo bila kuwasahau wanasiasa. Watu maarufu na mashuhuri hufaidika zaidi.
Wanamuziki na wanamichezo wananufaika zaidi kutokana na kuwa na wafuasi wengi katika mitandao tofauti ya kijamii. Idadi hiyo huongeza thamani ya mikataba mbalimbali wanayoingia. Idadi kubwa ya wafuasi kwa watu hawa ni mtaji wa biashara.
Hata kwa wanasiasa ina maana kubwa. Inaonyesha vitu viwili vikubwa; mosi, ni kwa namna gani mwanasiasa husika anakubalika katika jamii yake na pengine duniani kwa ujumla. Pili, ni kwa kiasi gani anajiweka karibu na wananchi. Mitandao ya kijamii inatoa fursa kwa mwanasiasa kuwasiliana na wafuasi wake moja kwa moja.
Ingawa wanamuziki ndiyo watu wanaoongoza kwa kuwa na wafuasi wengi katika mitandao hii duniani kote kwa ujumla, hali ni tofauti hapa nchini na Afrika Mashariki kwa jumla. Hilo limethibitishwa na utafiti uliofanywa na jarida la wiki la Mail & Guardian la Afrika Kusini lililoangalia ufuasi huo kwa Bara la Afrika pekee.
Matokeo ya utafiti
Utafiti huo uliotolewa hivi karibuni, unaonyeshsa kuwa mwanasiasa na Mbunge wa Kigoma Kaskazini, Zitto Kabwe anaongoza miongoni mwa Watanzania wanaotumia mitandao hiyo.
Previous
Next Post »