wa Simba, Hussein Shariff 'Casillas', amekata tamaa ya kurejea uwanjani msimu huu baada ya kushindwa kupona haraka jeraha la upasuaji wa mguu aliofanyiwa kufuatia kuumia wakati wa ziara ya mazoezi nchini Afrika Kusini.
Casillas aliyetua Simba akitokea Mtibwa Sugar ya Manungu, Turiani
mkoani Morogoro aliumia Desemba mwaka jana wakati timu hiyo ilipokuwa
ziarani 'Sauzi' na ana shaka kama ataweza kurejea kabla ya msimu huu
kumalizika Mei.
Akizungumza na gazeti hili jana, Casillas, alisema kwa sasa bado
anafanya mazoezi mepesi binafsi na uwanjani anakuwa pamoja na timu ya
vijana wa umri chini ya miaka 20 (Simba B).
"Bado naendelea na mazoezi, ila sijajua lini nitaweza kurejea
uwanjani, siwezi kujua kwa sasa mpaka pale kocha na daktari wa timu
watakaposema niko tayari," alisema kipa huyo.
"Ila ndiyo soka lilivyo, naamini nitarejea uwanjani na tena nitakuwa bora kuliko mnavyonifahamu," aliongeza.
Kutokana na Casillas na pia Ivo Mapunda kuwa majeruhi kwa nyakati
tofauti, kipa yosso Manyika Peter Jr. amekuwa akianza kwenye kikosi cha
kwanza cha timu hiyo ambayo sasa iko katika nafasi ya nne kwenye msimamo
wa ligi.
Kikosi cha Wekundu wa Msimbazi kilitarajiwa kuwasili mkoani
Shinyanga jana jioni tayari kuwakabili wenyeji Stand United katika
mchezo wa ligi utakaofanyika Jumapili kwenye Uwanja wa Kambarage.
CHANZO:
NIPASHE
Sign up here with your email
ConversionConversion EmoticonEmoticon