Straika BDF amkumbali Msuva“


“Kama wao wameweza kutufunga mabao mawili kwao kwanini sisi tushindwe kuwafunga kwetu? Beki yao pia nimeona siyo nzuri sana, kama tukicheza kwa kushambulia tunaweza kupata mabao mengi.
SHARE THIS STORY
0
Share


STRAIKA wa BDF XI, Vicent Nzombe, amesema winga Simon Msuva ni mchezaji tishio ndani ya Yanga, lakini ametamba kikosi chake kinaweza kubadili upepo kitakapocheza nyumbani ili kusonga mbele.
BDF ilifungwa mabao 2-0 na Yanga katika mechi ya kwanza ya Kombe la Shirikisho barani Afrika mchezo uliochezwa Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam juzi Jumamosi. Zitarudiana mbili zijazo huko Botswana.
Nzombe alisema Yanga iliweza kuwafunga mabao hayo kwa kutumia vizuri faida ya uwanja wa nyumbani jambo ambalo haliwakatishi tamaa kwani nao wanaweza kufanya hivyo watakapokutana katika mechi marudiano nyumbani kwao.
“Kwanza sikutarajia kama Yanga inacheza soka kiasi kile, nilidhani ni timu ya kawaida lakini kiwango walichokionyesha kimenishangaza kidogo, inabidi kujipanga kwa ajili ya mechi ya marudiano,” alisema.
“Kama wao wameweza kutufunga mabao mawili kwao kwanini sisi tushindwe kuwafunga kwetu? Beki yao pia nimeona siyo nzuri sana, kama tukicheza kwa kushambulia tunaweza kupata mabao mengi.
“Yule namba 27 (Simon Msuva) na kiungo wao mmoja wamecheza vizuri sana, walikuwa sumu kwa mabeki wetu na ninaweza kusema ndiyo wachezaji waliofanya vizuri zaidi kwa upande wa Yanga.
Previous
Next Post »