Yanga yamtanguliza mtaalamu Botswana

Kocha wa Yanga, Hans Pluijm alisema: “Walikuwa wengi nyuma katika mchezo wa Dar es Salaam, ilikuwa ngumu kuwafanya wafunguke ili tuweze kupita, tulichofanya mpaka tukawafunga zipo klabu nyingi Ulaya kinawashinda, lakini najua sasa nini tufanye tukiwa kwao.
SHARE THIS STORY
0
Share


BENCHI la Ufundi la Yanga limewashtukia BDF XI ya Botswana kwamba hawakucheza katika ubora wao, hivyo limemtanguliza haraka mtaalamu nchini humo ambaye atafanya ushushushu wa haraka na kukamilisha mipango yote.
Akizungumza na Mwanaspoti, Katibu Mkuu wa Yanga, Dk Jonas Tibohora, ambaye ana uelewa mkubwa wa masuala ya ukocha na ufundi, alisema benchi la ufundi la timu yao limemuagiza aondoke leo kuifuata timu hiyo kuwasoma watakapokuwa wakicheza mchezo wa LigiKuu Botswana kabla ya kurudiana na Yanga.
BDF XI ambayo juzi Jumamosi ilikubali kipigo cha mabao 2-0 katika mchezo wa kwanza wa Kombe la Shirikisho, keshokutwa Jumatano itashuka katika Uwanja wa SSKB kucheza na Orapa United katika ligi ya kwao.
Alisema mbali na jukumu hilo, pia atakuwa na kazi ya kufuatilia kila kitu kuhusu sehemu itakapofikia kikosi chao kwa mchezo wa marudiano.
“Kocha wetu ameona hilo kwamba kuna haja ya kumtuma mtu kutangulia huko na wakaona mimi niende nikafanye hiyo kazi ili niwape ripoti, tulitaka tumuagize Mkwasa (Charles) lakini kutokana na hizi mechi mbili za ligi tumeona abaki aongeze nguvu,” alisema Tibohora kuhusiana na kocha msaidizi huyo
Previous
Next Post »