Mtoto huyo aliibwa mbele ya wazazi wake, Jumapili wiki iliyopita,
majira ya saa 2.00 usiku, wakati akiwa amebebwa na mama yake, Esther
Bahati (30), baada ya kuvamiwa na kupigwa na mapanga na waporaji, akiwa
jikoni.
Kutokana na hali hiyo, TAS imeitaka jamii kushirikiana na Jeshi la
Polisi kuwafichua wahalifu hao, kwani hawatoki nje ya mkoa huo.
Msemaji wa TAS, Josephat Toner (pichani), alisema mfululizo wa
matukio ya kutekwa kwa watoto wenye ualbino nchini unasikitisha sana.
Alisema hadi sasa wakazi wa kijiji cha Ndami, Mkoa wa Mwanza bado
wana majonzi kutokana na kutekwa kwa mtoto, Pendo Emmanuel, Desemba 27
mwaka jana, ambaye mpaka sasa hajulikani aliko.
“Leo ni siku ya 52 bado mtoto Pendo Emmanuel hajapatikana,
limeibuka lingine. Kweli inasikitisha sana. Tunakosa amani ya maisha
yetu, hasa kwa watoto wetu, ambao hawawezi hata kujitetea,” alisema
Toner.
Alisema bado kuna haja kwa serikali kutoa elimu ya kutosha kwa
jamii ili kupata uelewa kuwa watu wenye ualbino hawana uhusiano na
utajiri, pia iwape ulinzi kutokana na mfululizo wa matukio ya kutekwa.
CHANZO:
NIPASHE
Sign up here with your email
ConversionConversion EmoticonEmoticon