Kikosi
cha timu ya Yanga kitaondoka nchini Alhamisi ijayo kuelekea Botswana
kwa ajili ya mechi yao ya marudiano ya hatua ya awali ya Ligi ya kombe
la Shirikisho Afrika. Yanga ilishinda 2-0 katika mechi yao ya kwanza
kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam Jumamosi.
Akizungumza na NIPASHE jana, Katibu Mkuu wa Yanga, Dk. Jonas
Tiboroha, alisema kikosi hicho kitaondoka jijini kikiwa na wachezaji
wote watakaokuwa wazima.
Alisema kwa sasa wachezaji wote wako imara na tayari wapo jijini
Mbeya kwa ajili ya kujiandaa na mechi yao ya kesho dhidi ya Prisons ya
huko na ya Jumapili dhidi ya Mbeya City kwenye Uwanja wa Sokoine.
Alisema tayari maandalizi mazito yanaendelea kuhakikisha kwamba
wanashinda mechi yao ya marudiano dhidi ya BDF XI na kutinga katika
hatua ya kwanza.
CHANZO:
NIPASHE
Sign up here with your email
ConversionConversion EmoticonEmoticon