Baraka Kizuguto, Ofisa Habari wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF),
alisema jijini Dar es Salaam jana kuwa wawili hao wamechaguliwa na jopo
la makocha kutokana na mchango wao mkubwa kwenye timu zao katika mwezi
husika.
Kizuguto alisema Mahundi anayeshikilia rekodi ya kufunga bao la
mapema zaidi msimu huu, alitoa mchango mkubwa kwa timu yake ya Coastal
Union mwezi Desemba mwaka jana.
Hata hivyo, mabingwa hao wa 1988 wa Tanzania Bara, walicheza mechi
moja tu Desemba wakitoka suluhu dhidi Tanzania Prisons kwenye Uwanja wa
Kumbukumbu ya Sokoine jijini Mbeya Desemba 27, mwaka jana.
Ofisa Habari huyo aliendelea kueleza kuwa Bahanunzi, mfungaji bora
wa Kombe la Kagame 2012 (mabao 6) anayechezea Polisi Moro kwa mkopo
akitokea Yanga, amekuwa na mchango mkubwa kwa timu yake hiyo mpya tangu
ajiunge nayo kwenye kipindi cha usajili cha "dirisha dogo" msimu huu.
Mwezi uliopita (Januari), Polisi Moro inayonolewa na Adolf Richard,
ilikusanya pointi sita katika mechi nne, ikishinda 1-0 dhidi ya Mbeya
City, sare dhidi ya Ndanda FC, Coastal Union na Stand United na kupoteza
1-0 dhidi ya Yanga.
Katika mechi hizo, Bahanunzi alifunga mabao mawili yaliyowapa
ushindi wa 1-0 nyumbani mjini Morogoro dhidi ya Mbeya City Januari 31
lililoipaisha timu yake hadi katika nafasi ya tatu katika msimamo wa
ligi, na sare ya 1-1 ugenini mjini Mtwara dhidi ya Ndanda FC Januari 10.
"Kwa kuibuka wachezaji bora, Mahundi na Bahanunzi watazawadiwa
fedha taslimu Sh. milioni moja kila mmoja kutoka kwa wadhamini wakuu wa
ligi hiyo, Kampuni ya Huduma za Mawasiliano ya Vodacom Tanzania,"
alisema Kizuguto.
Sign up here with your email
ConversionConversion EmoticonEmoticon