Wito huo umetolewa na mwenyekiti wa Chama cha Soka mkoani Mtwara
(MTWAREFA), Athumani Kambi, wakati alipokuwa akifanya mahojiano maalumu
na NIPASHE na kusema kuwa, kwa sasa mbunge wa Mtwara vijijini, Hawa A.
Ghasia, ndiyo anayeisaidia timu hiyo.
Kambi alisema kuwa tangu wamepanda daraja mpaka hapo walipo sasa hawajapokea msaada wowote kutoka kwa wabunge wengine.
"Sisi tupo na hatuna upande, mbunge akileta msaada tutaupokea,”
alisema Kambi na kuongeza kuwa, “sisi mtu yoyote anayetuletea msaada
tunatangaza, kwa mfano hivi sasa Mbunge wa Mtwara vijijini analipa posho
kwa wachezaji na tunatangaza,” aliongeza.
Alisema awali, Mbunge wa Mtwara Mjini, Asnain Murji, alikuwa anatoa
mabasi yake kwa kuchangisha kiasi fulani cha pesa kuwasafirisha
mashabiki kwenda kuishangilia timu pindi inapokwenda kucheza ugenini
lakini kwa sasa huduma hiyo ameisitisha japo alifanya tena hivyo
walipokwenda kucheza dhidi ya Yanga Dar es Salaam na kutoka suluhu.
Habari za ndani zinasema Ghasia, ambaye pia ni Waziri wa Tamisemi,
anatoa posho kwa wachezaji kila wiki kiasi cha Sh. milioni 1.2.
Kiuhalisia, timu ya Ndanda haijapata matokeo ya kuridhisha katika
mechi zake za kwenye uwanja wa nyumbani wa Nangwanda Sijaona isipokuwa
mechi moja pekee waliyoshinda 1-0 dhidi ya Azam Novemba 1, mwaka jana.
Mechi iliyopita dhidi ya Mtibwa Sugar ilikuwa ni mechi yao ya 15 ya
Ligi Kuu msimu huu, na kati ya hizo mechi saba wamecheza nyumbani na
kushinda moja tu, mechi tatu wamefungwa ambazo ni dhidi ya Ruvu Shooting
3-1, JKT Mgambo 1-0 na Simba 2-0. Mechi walizotoa sare ni tatu, ambazo
ni dhidi ya Polisi Moro 1-1, Stand United 1-1 na Mtibwa Sugar 0-0, na
katika msimamo wa ligi wanashika nafasi ya 11 wakiwa na pointi 16.
Mechi inayofuata, Ndanda watacheza dhidi ya Coastal Union ya Tanga Februari 21, 2015 kwenye uwanja wao wa Nangwanda Sijaona.
CHANZO:
NIPASHE
Sign up here with your email
ConversionConversion EmoticonEmoticon