Habari kutoka klabuni hapo zinasema staa huyo wa
kimataifa wa Argentina alipatiwa matibabu ya awali uwanjani hapo, lakini
ameibua hofu kwamba huenda akawa ametonesha nyonga, tatizo lililomweka
nje ya uwanja wakati wa Krismas
style="display:inline-block;width:680px;height:300px"
data-ad-client="ca-pub-3992075039970891"
data-ad-slot="7646462965">
style="display:inline-block;width:680px;height:300px"
data-ad-client="ca-pub-3992075039970891"
data-ad-slot="7646462965">
Kutoka na wasiwasi huo, Di Maria anaweza kupumzishwa kwa ajili ya kufanyiwa uchunguzi zaidi.
Kikosi hicho cha kocha, Louis van Gaal, Jumamosi
kitakuwa na mechi ya ugenini dhidi ya Swansea City na uwezekano wa staa
huyo kucheza upo mashakani kutokana na hali hiyo.
Nyota huyo wa zamani wa Real Madrid aliyeianza
Ligi Kuu England kwa kasi alipofunga mabao matatu na kusababisha mengine
manne katika mechi sita za awali, katika miezi ya karibuni amekuwa na
wakati mgumu akifunga mara moja tu katika michezo 16.
Kuumia kwa Di Maria kunaongeza hofu kwa kocha
Mholanzi Van Gaal hasa kwa kuwa Phil Jones na Michael Carrick nao pia
wapo katika benchi la majeruhi. Hata hivyo, kocha huyo anapumua kutokana
na habari kuwa straika, Robin van Persie, amepona matatizo yake
yaliyomkosesha mechi ya Kombe la FA dhidi ya Preston North End na
anatarajiwa kuivaa Swansea
Sign up here with your email
ConversionConversion EmoticonEmoticon