Tambwe alifunga mabao hayo kwa ustadi mkubwa baada
ya kuwazidi ujanja mabeki wa BDF na kutumia nafasi mbili kubwa
alizopata kuleta madhara kwa wapinzani hao na kuiweka Yanga katika
nafasi nzuri ya kusonga mbele katika michuano hiyo ya Afrika.
Mabao hayo mawili ni mwendelezo wa kazi nzuri
anayoifanya Tambwe katika kikosi cha Yanga tangu alipojiunga na mabingwa
hao wa kihistoria wa Ligi Kuu Bara kwenye usajili wa dirisha dogo,
Desemba mwaka jana.
Straika huyo raia wa Burundi alifanikiwa kujiunga
na Yanga siku ya mwisho ya dirisha la usajili baada ya kuvunjiwa mkataba
wake na Simba aliyokuwa ameitumikia kwa msimu mmoja na nusu. Moja ya
mafanikio makubwa ya Tambwe akiwa Simba ni kuibuka mfungaji bora wa
msimu uliopita na kuiwezesha timu yake iliyokuwa na mwenendo wa kusuasua
kumaliza katika nafasi ya nne.
Kuachwa kwa Tambwe kulizua mjadala mrefu Simba juu
ya uhalali wa sakata hilo lakini siasa zilitumika na kudai kuwa straika
huyo hana mpya la kuisaidia Simba licha ya kwamba anafanya makubwa
Jangwani kwa sasa.
style="display:inline-block;width:680px;height:300px"
data-ad-client="ca-pub-3992075039970891"
data-ad-slot="7646462965">
style="display:inline-block;width:680px;height:300px"
data-ad-client="ca-pub-3992075039970891"
data-ad-slot="7646462965">
Achana na Tambwe, Mwanaspoti inakuletea orodha ya mastaa wengine wa Simba waliofanikiwa kung’ara na kikosi cha Yanga.
Kelvin Yondani
Beki wa Kati wa Yanga, Kelvin Yondani naye
alijiunga na timu hiyo akitokea Simba ambapo mkataba wake ulimalizika.
Taarifa za ndani ya Simba kwa wakati huo zilieleza kuwa, klabu hiyo
ilishindwa kumwongezea mkataba Yondani kwa madai ya kushuka kwa kiwango
pamoja na kuihujumu timu hiyo. Yondani kwa wakati huo alikuwa amecheza
kwa misimu minne mfululizo na Simba na kuwemo kwenye kikosi kilichotwaa
ubingwa wa ligi mwaka 2010 na 2012. Hata hivyo, licha ya madai hayo ya
Simba, Yondani amekuwa nguzo muhimu katika kikosi cha Yanga tangu
alipojiunga mwaka 2012 na amekuwa hakosekani katika kikosi cha kwanza
cha makocha wote waliopita klabuni hapo. Beki huyo amefanikiwa
kutengeneza kombinesheni ya maana na Nadir Haroub ‘Cannavaro’ na
kuifanya safu ya ulinzi ya Yanga kuwa ya kuogopeka.
Juma Kaseja
Achana na kipa Juma Kaseja aliyetua Yanga mwaka
2013. Hapa anazungumziwa Kaseja aliyetua Yanga msimu wa 2008/09 wakati
huo akiwa moto wa kuotea mbali. Kaseja alijiunga na Yanga kwa mkataba wa
mwaka mmoja kwa kipindi hicho, baada ya kumaliza mkataba wake na Simba
na kuwa nguzo muhimu kwenye kikosi cha Yanga kilichotwaa ubingwa msimu
huo. Kutua kwa Kaseja kwenye kikosi cha Yanga kwa msimu huo kuliwashtua
wengi lakini alirejea Simba baada ya kumalizika kwa msimu, hivyo
kuwatuliza mashabiki wa timu hiyo waliokuwa wameanza kuhamaki.
Emmanuel Okwi
Mshambuliaji Emmanuel Okwi raia wa Uganda
aliifungia Yanga bao la kufutia machozi katika kipigo cha mabao 3-1
kutoka kwa Simba katika pambano la Nani Mtani Jembe mwaka 2013. Hiyo
ilikuwa ni mechi ya kwanza ya Okwi katika kikosi cha Yanga baada ya
kujiunga na klabu hiyo katika siku ya mwisho ya usajili wa dirisha dogo
Desemba 15 mwaka huo. Mashabiki wa Simba walikuwa hawaamini kilichotokea
hasa baada ya kupata taarifa kuwa mabosi wa klabu yao walikuwa
wakihangaika kumrejesha Okwi kundini.
Sign up here with your email
ConversionConversion EmoticonEmoticon