Baada ya miaka 27, Mwadui FC imerejea Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania
Bara (VPL) kutokana na kumaliza nafasi ya kwanza katika Kundi la Ligi
Daraja la Kwanza (FDL) msimu huu.
Akizungumza na NIPASHE akiwa Shinyanga jana, Julio alisema: "Mimi
ni kocha fundi, nimepanda Ligi Kuu na ninakuja kupambana. Siji kushiriki
ligi.
"Msimu ujao hakuna cha Yanga, Simba wala Azam. Nitamaliza katika nafasi tatu za juu. Tuna timu nzuri na uongozi imara.
"Kama Mungu kapanga, kapanga tu. Tulianza kwa kusuasua dhidi ya
Panone FC, Toto Africans na Oljoro JKT, lakini baadaye tukawa tunashinda
tu.
"Ukisikia mtu anaoa ujue kajipanga maana baada ya kufunga ndoa kuna
watoto na ada za shule. Kupanda kwetu Ligi Kuu ni sawa na kuoa,
tumejipanga kupambana.
"Toto ilitusumbua sana maana tulikuwa tunabadilishana nayo kukaa
kileleni mwa msimamo," alisema zaidi kocha huyo wa zamani wa Tanzania
Stars na Simba.
Mwadui FC yenye maskani yake kwenye Migodi ya Almasi ya Mwadui
mkoani Shinyanga, imeungana na timu nyingine tatu; Toto Africans ya
Mwanza, Africans Sports ya Tanga na Majimaji FC ya Ruvuma kupanda VPL
msimu ujao. Timu zote nne ziliwahi kushiriki ligi hiyo.
Timu mbili zitakazomaliza nafasi za chini VPL msimu huu, zitashuka
daraja kuzipisha timu hizo nne, hivyo kuongeza idadi ya timu shiriki za
ligi kuu kutoka 14 hadi 16.
Sign up here with your email
ConversionConversion EmoticonEmoticon